Man city yazindua Jezi mpya zitakazo tumika msimu ujao (Picha)
Klabu ya Manchester City ya nchini Uingereza imetangaza rasmi Jezi zake
mpya zitakazo tumika katika msimu ujao wa ligi wa mwaka 2017/18, klabu
hiyo yenye maskani yake Etihad, imeweka hadharani uzi wao utakao
tumika katika vikosi vyote, timu ya wakubwa kwa upande wa wanaume na
wanawake, timu ya vijana na zile za watoto.