Header Ads

PropellerAds

Breaking News

KIGOGO CHADEMA ACHEZEA KICHAPO TOKA KWA WANACHAMA


KATIBU wa muda wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Wilaya ya Kyela, Mponjoli Mwaikimba, amenusurika kufa baada ya kuvamiwa na kundi la wanachama walioingia kwenye ofisi za chama na kumpiga na kumsababishia maumivu makali.
Patashika hiyo ilitokea jana saa tano asubuhi wakati katibu huyo akiwa ofisini kwake makao makuu ya Chadema wilaya, mjini hapa. Wanachama hao waliingia ndani na kuanza kumcharaza makofi na baadaye kumwacha akiwa hoi.

Mwenyekiti wa muda wa chama hicho wilayani hapa, Philemon Mahenge, alisema alipata taarifa za uvamizi huo na alipofika ofisini, wavamizi walikuwa wametokomea ndipo alipochukua jukumu la kwenda kumpeleka polisi kutoa maelezo na baadaye kupewa fomu ya matibabu na kumpeleka hospitalini.
Alisema kitendo kilichofanywa na watu hao, hakivumiliki na kuwa walipotoa ripoti polisi na kuwataja baadhi ya wanachama waliohusika, wanachama wawili walikamatwa huku wengine wakiendelea kutafutwa.