Header Ads

PropellerAds

Breaking News

Maamuzi ya mwisho ya Man United kuhusu ajira ya Louis van Gaal yametangazwa leo May 23 2016

Baada ya headlines za muda mrefu kuhusu ajira ya kocha wa Man United Louis van Gaal kuripotiwa kuwa mashakani, huku uongozi wa Man United ukiwa umekaa kimya pasipo kukanusha au kukubali habari hizo, leo May 23 2016 taarifa rasmi zimetoka.
Taarifa rasmi iliyoripotiwa na dailymail.co.uk na BBC Sports inaeleza maamuzi ya klabu hiyo yamefikiwa mchana wa leo na kuamua kumfuta kazi Louis van Gaal, kocha huyo wa kiholanzi anapoteza kazi ikiwa ni siku mbili zimepita toka ashinde Kombe la FA na klabu hiyo.
Van Gaal amefukuzwa lakini ameripotiwa Jose Mourinho kujiandaa kuchukua nafasi yake muda wowote kuanzia hivi sasa, Van Gaal ameondoka pamoja na kocha msaidizi Albert Stuivenberg na kocha wa makipa Frans Hoek, hivyo Mourinho atakuja na benchi jipya la ufundi.