Header Ads

PropellerAds

Breaking News

Hivi hapa Vyuo 1000 Bora Duniani, Afrika vipo 14

June 4, 2018 Vyuo 14 tu kutoka bara la Afrika katika nchi za Afrika Kusini 7, Misri 4, Nigeria 1, Tunisia 1 na Uganda 1 ndio vimeingia katika orodha ya vyuo 1000 bora Duniani, hili limebainishwa katika orodha ya vyuo bora Dunia ya mwaka 2018 iliyotolewa na Center for World University Rankings(CWUR).
 
CWUR inapima ubora wa elimu na mafunzo kwa wanafunzi, ufahari wa wanafunzi walio katika vitivo mbalimbali pamoja na ubira wa tafiti bila kutegemea ‘data’ zilizokusanywa na chuo husika.

Marekani ina jumla ya vyuo 8 katika Kumi bora, huku Chuo Kikuu Harvard kikishika namba 1 kwa mwaka wa 7 mfululizo sasa. Chuo hicho kinafwatiwa na Chuo Kuu cha Stanford, Chuo cha Ufundi Massachusetts, Chuo Kikuu cha Cambridge, Chuo Kikuu Oxford, Chuo Kikuu cha California, Berkeley, Chuo Kikuu Princeton, Chuo Kikuu Columbia, Chuo cha ufundi California na Chuo Kikuu cha Chicago.
Katika vyuo kutoka Afrika Kusini, Chuo Kikuu cha Cape Town kimeshika nafasi ya 223 huku ndio kikiwa Chuo cha kwanza Afrika, kimefwatiwa na Chuo Kikuu cha Witwatersrand(230), Chuo Kikuu cha KwaZulu-Natal(402), Chuo Kikuu cha Pretoria(438), Chuo Kikuu Stellenbosch(448), Chuo Kikuu cha Johannesburg(790) na Chuo Kikuu North-West(964).
 
Katika vyuo kutoka Misri, Chuo Kikuu Cairo kimeshika namba 452, kikifwatiwa na Chuo Kikuu Ain Shams(715), Chuo Kikuu Mansoura(884) na Chuo Kikuu Alexandria(903).

Chuo kutoka Uganda, Chuo Kikuu Makerere kimeshika nafasi ya 771, Chuo Kikuu Tunis El Manar kutoka Tunisia kimeshika nafasi ya 908 wakati Chuo cha Ibadan kutoka Nigeria kikishika nafasi ya 991.