Header Ads

PropellerAds

Breaking News

Ushauri wa Wataalam kuhusu Mchanga wa madini

Chama cha ACT Wazalendo kilifanya Kongamano kuhusu Rasilimali Madini ambalo lilifanyika katika Ukumbi wa Makumbusho ya Taifa DSM kujadili masuala yanayohusu madini likiwemo Mchanga wa Madini uliokuwa unasafirishwa nje ya nchi ambao sasa umezuiwa.
Wataalam mbalimbali wa masuala ya madini na wafanyakazi wa migodini walikuwa ni miongoni mwa walipata nafasi ya kuchangia hoja katika Kongamano hilo ambapo mmoja kati yao ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Migodini Nicomeds Kajungu.
“Baada ya kuwa tumesikia kwamba kuna katazo la Serikali kwamba makenikia au mashobo yasisafirishwe tena, sisi kama Wafanyakazi tuiona ni muhimu sana kwa sababu ni wadau wakubwa sana…” – Nicomedes Kajungu.
Unaweza kutazama kwa kuplay VIDEO hii ambayo ina kila kitu kuhusu ushauri wa wataalam wa Madini ambao wameshauri nini kifanyike juu ya Mchanga wenye Madini uliozuiwa kwenda nje ya nchi…