Header Ads

PropellerAds

Breaking News

USAJIRI BALANI ULAYA NA DILI ZILIZO KAMILIKA

MAN UTD TO YAFUFUA UPYA NIA YA KUMSAJILI GRIEZMANN
Manchester United huenda wakafufua upya lengo lao kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoine Griezmann, klabu hiyo ikiwa inahaha kuipata saini ya Alvaro Morata wa Real Madrid pia, kwa mujibu wa Metro

ARSENAL YAKUBALI OFA ZA OSPINA

 
Fenerbahce wamefikia makubaliano na Arsenal kwa ajili ya kipa David Ospina, kwa mujibu wa  Fanatik .Kipa huyo wa kimataifa wa Colombia atauzwa kwa paundi milioni 3 na atapaa hadi Uturuki kukamilisha vipimo vya afya na kusaini dili la miaka minne.

 RONALDO KUTIMKIA CHINA KWA €200M
Cristiano Ronaldo anaweza kutolewa dau la euro milioni 200 na klabu moja inayoshiriki Ligi Kuu ya China, kwa mujibu wa ripoti kutoka  AS .
Mreno huyo amekuwa gumzo katika tetesi zilizomhusisha na klabu za China, ingawa alitupilia mbali tetesi hizo akisisitiza anataka kubaki Real Madrid.Sasa, Licha ya kuwa na mkataba na Real hadi 2021, inaaminika Ronaldo amepokea ofa ya euro milioni 200 na atalipwa euro milioni 120 kwa mwaka katika ujira wake.

PSG YAONGOZA MBIO ZA KUMSAJILI JAMES

 PSG inaongoza katika mbio za kumsajili James Rodriguez wa Real Madrid, kwa mujibu wa France Football .
Mchezaji huyo raia wa Colombia anatafuta klabu itakayompa muda wa kutosha kucheza, klabu kubwa kama Manchester United, Arsenal na Chelsea zinaitamani saini yake lakini miamba hao wa Ufaransa wanaelekea kushinda mbio hizo za kumsajili.