Header Ads

PropellerAds

Breaking News

TETESI ZA USAJIRI BARANI ULAYA

BAYERN KUMLIPA ALEXIS €480K KWA WIKI

 
Bayern Munich wapo tayari kumfanya Alexis Sanchez kuwa mchezaji anayelipwa zaidi, na watamlipa euro 480,000 kwa wiki, kimeripoti  Kicker .
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Chile anataka kuondoka Arsenal, na Bayern na Manchester United zinaitaka huduma yake, lakini miamba wa Bundesliga wapo katika nafasi nzuri zaidi kumsajili.

UNITED YAONGEZA OFA YA MORATA


Manchester United wameongeza ofa yao kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata hadi paundi milioni 60, kwa mujibu wa The Guardian .
Mashetani Wekundu walishuhudia ofa yao ya awali ya paundi milioni 52 ikitoswa na miamba hao wa Hispania.

MADRID HAWATAMNUNUA DE GEA

 
Real Madrid wameamua kuachana na kipa wa Manchester United David De Gea, kwa mujibu wa Marca .

CHELSEA KUMLIPA LUKAKU ZAIDI YA COSTA

 
Chelsea wapo tayari kumlipa Romelu Lukaku mshahara mnono kuliko Diego Costa ili waweze kumsajili tena mshambuliaji huyo mahiri wa Everton, kimeripoti Liverpool Echo .
Costa amedai kuwa hatakiwi tena na Antonio Conte na bosi huyo wa Chelsea anamtaka Lukaku kama mbadala wake.