Header Ads

PropellerAds

Breaking News

TCRA wafanya ukaguzi wa mwisho na kuiruhusu Radio5 kurudi hewani Disemba 16

Mamlaka ya Mawasiliano nchini Tanzania TCRA, leo December 14 imefanya ukaguzi wa mwisho, kujiridhisha na kuruhusu kituo cha utangazaji cha Radio5 Arusha kurudisha matangazo yake hewani ifikapo Disemba 16 mwaka huu 2016.

Akiongea na viongozi na baadhi ya wafanyakazi wa Radio5 baada ya kukamilisha ukaguzi wao, Mkurugenzi wa Utangazaji wa TCRA Fredrick Ntobi amesema wao kama Mamlaka waliamua kuja kufanya ukaguzi wao kwa ajili ya kujiridhisha kurudisha matangazo ya kituo hicho hewani December 16 ambapo ndiyo tarehe rasmi ya kuisha kwa Adhabu waliyokuwa wamewapa Kituo hicho.

Mamlaka hiyo ilifanya ukaguzi wa studio ya kurusha matangazo (On air Studio), studio ya kuzalisha vipindi (Production Studio), chumba cha Habari (News room), control Room, ofisi zote za kituo pamoja na mnara wa kurushia matangazo ambapo kote wamekuta kila kitu kiko sawa kwa kazi kama mamlaka inavyotaka.
Hata hivyo Fredrick Ntobi akiwa ameongozana na viongozi wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA kanda ya Kaskazini, amewakumbusha watangazaji na waandishi kufuata maadili ya uandishi wa habari ili kulinda Vvituo vyao na kulinda taaluma zao kwa ajili ya kuendelea kuhabarisha na kuelimisha Jamii nzima ya Watanzania.
Hata hivyo Fredrick Ntobi akiwa ameongozana na viongozi wa mamlaka ya mawasiliano Tanzania TCRA kanda ya Kaskazini, amewakumbusha watangazaji na waandishi kufuata maadili ya uandishi wa habari ili kulinda Vvituo vyao na kulinda taaluma zao kwa ajili ya kuendelea kuhabarisha na kuelimisha Jamii nzima ya Watanzania.
Naye Mkurugenzi wa Tan Communication Media inayomiliki kituo cha Radio5, Robert Francis, amewataka Wasikilizaji wa Radio5 kukaa mkao wa kuhabarika, kupata burudani na kuelimika zaidi kupitia Radio5 kwani wamejipanga vyakutosha kurudi hewani kwa kishindo.