Header Ads

PropellerAds

Breaking News

TETESI ZA USAJIRI MAJUU:MAN UTD YATAKIWA KUTOA £50M KUMSAJILI DIER

Manchester United wameambiwa watoe paundi milioni 50 au zaidi kumsajili kiungo wa Tottenham Eric Dier, Telegraph  limeripoti.
Jose Mourinho anataka mchezaji huyo wa Spurs asajiliwe kabla ya msimu mpya kuanza, lengo ni kutafuta mrithi wa kudumu wa Michael Carrick.

MENDES AIAMBIA REAL RONALDO ANA OFA KUTOKA UINGEREZA

Wakala wa Cristiano Ronaldo, Jorge Mendes ameiambia Real Madrid kuwa mshambuliaji huyo amepokea ofa kadhaa kutoka klabu za Ligi ya Uingereza, kwa mujibu wa  Cope  

MAN UTD & JUVE ZAMFUATILIA GOMES
Manchester United na Juventus zinafuatilia maendeleo ya kiungo wa Barcelona Andre Gomes, kwa mujibu wa habari za  AS .
Gomes amekuwa na mwanzo mgumu Barcelona na Mreno huyo anaweza kutimkia kwenye klabu mojawapo kati ya Juventus na Manchester United.

BAKAYOKO AAMUA KUTUA CHELSEA

Kiungo wa Monaco, Tiemoue Bakayoko amechagua kujiunga na Chelsea badala ya Manchester City na Man United, kwa mujibu wa  L'Equipe, kupitia Sport Witness .