Header Ads

PropellerAds

Breaking News

P – Funk akirudi rasmi kwenye muziki moto utawaka – Mr Ttouch

Mtayarishaji wa muziki ambaye anafanya vizuri kwa sasa, Mr Ttouch kutoka Touchz Sounds, hivi karibuni alimtembelea mtayarishaji mkongwe wa muziki P-Funk Majani kutoka Bongo Record na kupiga naye stori kuhusu tasnia ya muziki. 

Akiongea na Bongo5 Ijumaa hii, Mr Ttouch amedai alimtembelea producer huyo kwaajili ya kumtakia hali kwa kuwa ni mtayarishaji mkongwe ambaye anazifuatilia kazi zake kwa muda mrefu.
“P Funk nilimtembelea kumtakia hali tu kwa sababu ni producer ambaye namfuatilia sana toka zamani, kwahiyo hakuna chochote kinachoendeleza kati yetu,” alisema Ttouch. “Binafsi ukimya wa P-Funk naona kama kuna kitu tunakikosa kwenye game, P-Funk ni mtu mwingine kwenye muziki naona kama kweli angekuwa anaendelea kufanya project kama zamani game ya muziki ingechangamka,”
Touch alisema bado hajapata nafasi ya kufanya kazi ya pamoja na mkongwe huyo.